Thursday, August 9, 2012

HIVI NDIVYO VIWANGO VYA UBORA WA SOKA VYA FIFA - SPAIN KILELENI - ENGLAND YA TATU - BRAZIL YAZIDI KUSHUKA - TANZANIA NAFASI MOJA CHINI


Timu ya Taifa ya Spain imeendelea kukalia kiti cha uongozi wa ubora wa soka kwa mujibu wa viwango vya FIFA. Mabingwa ha wa dunia na ulaya wameshikilia uongozi huo wakiwa na pointi 1605, nafasi ya pili imekamatwa na Ujerumani, England wameendelea kupanda ubora kwenye rank hizo za FIFA bada ya mwezi uliopita kushika nafasi ya nne.

Brazil mabingwa wa mara tano wa dunia wameendelea kuweka rekodi, baada ya kushika nafasi ya chini zaidi katika historia yake, wakikamata nafasi 13, ikiwa ni mara ya kwanza kushuka kwa namna hiyo.

Ivory coast ndio pekee ya kiafrika kuwemo ndani ya 20 bora, wakishika nafasi ya 16. Timu ya taifa ya Tanzania imeshuka kwa nafasi moja kutoka nafasi ya 127 mpaka 128.







            












0 comments:

Post a Comment