Friday, August 24, 2012

Viwanjani Leo Ijumaa-Yanga Kucheza Na Rayon ya Rwanda Leo


Rais Paul Kagame katika picha ya pamoja na Yanga. (Picha  na Saleh Ally wa gazeti la Champion).
Mabingwa wa Kombe la Kagame klabu ya Dar Young Africans  leo watashuka dimbani kuivaa Rayon Sports ya Rwanda kwenye Uwanja wa Amaholo jijini Kigali.

Ufafanuzi Oparesheni Ya Kuwaondoa Wavamizi Wa Ardhi Eneo La Madale Na Zoezi La Sensa Jijini Dar Watolewa.


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kufafanua oparesheni ya kuwaondoa wavamizi wa ardhi katika eneo la Madale na zoezi la Sensa ya watu na makazi leo jijini Dar es salaam.

Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
 
Serikali imesema kuwa haitayavumilia makundi ya watu wanaovunja sheria za nchi kwa kuendesha vitendo vya wizi, uvunjaji wa nyumba, uporaji na uuzaji wa ardhi kinyume cha sheria katika maeneo yanayomilikiwa kihalali jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw. Saidi Meck Sadiki ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam kufuatia vurugu zilizotokea katika eneo la Madale nje kidogo ya jiji la Dar es salaam kutokana na uamuzi wa serikali kuwaondoa kwa nguvu wananchi waliovamia maeneo hilo.
Amesema kuwa serikali haikukurupuka kuchukua hatua hiyo na kuongeza kuwa hatua zilizochukuliwa zimezingatia kanuni na taratibu za kisheria zikiwemo baraka za kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.
“ Kufanyika kwa zoezi hili si kwamba serikali ya Kinondoni imekurupuka, hata kidogo haijafanya hivyo, zoezi hili limefuata kanuni na taratibu zote za kisheria ikiwemo uamuzi wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Dar es salaam na amri ya Mahakama”
Amefafanua kuwa matukio yaliyotokea hivi karibuni katika maeneo hayo kwa baadhi ya makundi ya wananchi hasa vijana waliobeba silaha za jadi kuwashambulia, kuwajeruhi na kuharibu mali za wananchi wanaoishi katika eneo la Madale kihalali kwa lengo la kuwaondoa kwa nguvu na kuyatwaa maeneo yao ni jambo lisilokubalika nchini.
Amesema kuwa licha ya jambo hilo kuwa la muda mrefu na serikali kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kihalali wanafanya shughuli zao bila kusumbuliwa baadhi ya wananchi wamekuwa hawakubaliani na jambo hilo na hatimaye kuanza kuyavamia maeneo ya wazi ambayo mengine yanamilikiwa na taasisi na makampuni.
Ameongeza kuwa zoezi hilo la kuwaondoa wananchi waliovamia maeneo hayo lilizingatia taratibu zote ikiwemo hatua ya serikali kuwapa taarifa wahusika wote waliovamia maeneo hayo kuondoka wenyewe jambo ambalo hawakulifanya.
“Kabla ya kutumia nguvu kuwaondoa wananchi hao serikali iliwapatia taarifa ya kuwataka kuondoka wenyewe jambo ambalo walilikaidi na kuendelea kukalia maeneo hayo kinyume cha sheria.
“ Bado naendelea kusisitiza kuwa serikali ilifuata taratibu zote, kwanza tuliwashauri wamiliki halali kwenda mahakamani kisha mahakama ikatoa amri ya wavamizi hao kuondolewa na zaidi ya hapo walipewa taarifa ya kuondoka wao wenyewe jambo ambalo hawakulifanya na hii inaashria kudharau amri ya mahakama” amesisitiza Bw. Sadiki.
Aidha Bw. Saidi Meck Sadiki amesema kuwa imebainika kuwa baadhi ya wananchi wanaoendesha vitendo hivyo vya kihalifu sio raia wa Tanzania na kukongeza kuwa tayari vyombo vya dola vinavyohusika vinaendelea na uchunguzi wa suala hilo na tayari vinawashikilia watu 68 kwa kuhusika na vurugu hizo.
Pia ameonyeshwa kusikitishwa na baadhi ya watendaji wachache wa serikali na viongozi wa siasa wanaoshabikia na kuhamasisha suala hilo na kuongeza kuwa serikali inaendelea na uchunguzi wa suala hilo na ikibainika hathua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amevipongeza vyombo mbalimbali vya habari vinavyoendelea kuwahamasisha wananchi kushiriki katika zoezi la Sensa ya watu na makazi na kuongeza kuwa hivi sasa wananchi wana uelewa mkubwa juu ya zoezi hilo na wako tayari kuhesabiwa.
“Navishukuru sana vyombo vya habari kwa kazi nzuri za uhamasishaji wa watu kushiriki katika Sensa ya watu na Makazi japo vipo vichache sana vinavyoendesha mijadala ya kuipinga”

MBUYI TWITE ATHIBITISHWA RASMI NA TFF KUJIUNGA NA YANGA


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa wachezaji 11 wa nje kati ya 14 walioombea usajili na klabu mbalimbali za Ligi Kuu.
 
Wachezaji walioombewa usajili Yanga na tayari ITC zao zimepatikana ni Nizar Khalfan kutoka Vancouver Whitecaps ya Canada, Didier Kavumbagu (Atletico Olympic- Burundi) na Mbuyu Twite kutoka FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
 
Kwa upande wa Simba ni Musa Mude (Sofapaka, Kenya) na Daniel Akuffor (Stella Abidjan, Ivory Coast) wakati Mtibwa Sugar ni Shabani Kisiga timu ya El Itihad ya Oman.
 
Waliopata ITC kwa upande wa Kagera Sugar ni Wilfred Ojodale Ame na Benjamin Efe Ofuyah wote kutoka FC Abuja ya Nigeria. Wengine ni Deangelis Silva kutoka New Road ya Nepal kwenda Coastal Union, George Odhiambo kutoka Randers FC ya Denmark kwenda Mtibwa Sugar na Jerry Santo kutoka Tusker, Kenya kwenda Coastal Union.
 
Wachezaji ambao wameombewa usajili na ITC zao bado hazijapatikana ni Salum Kinje na Pascal Ochieng wa AFC Leopards, Kenya kwenda Simba na Ayoub Hassan Isiko kutoka Bull FC, Uganda kwenda Mtibwa Sugar.
 
Bado klabu ambazo hazijakamilisha usajili na kupata ITC zina fursa ya kufanya hivyo hadi Septemba 4 mwaka huu ambapo dirisha litafungwa.
 
Pia TFF imetoa ITC kwa wachezaji wanane walioombewa kwenda kucheza mpira wa miguu katika nchi za Kenya na Msumbiji kutoka katika klabu mbalimbali za hapa nchini.
 
Wachezaji hao na klabu wanazokwenda katika mabano ni Abdallah Ally Abdallah (CD Madchegde, Msumbiji), Almasi Khatib Mkinda (Ferroviario da Beira, Msumbiji), David Naftali (Bandari, Kenya) na Hassan Hassan Mustafa (CD Madchegde, Msumbiji).
 
Wengine ni Meshack Abel (Bandari, Mombasa), Mohamed Banka (Bandari, Kenya), Thobias Davis Silas (CD Madchegde, Msumbiji) na Thomas Maurice (Bandari, Kenya).

Simba, Azam Zajiandaa Kwa Ajili Ya Ngao Ya Hisani Septemba 8

Kikosi cha Simba.


Kikosi cha Azam.


KATIKA kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii, mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC, Jumamosi watacheza mechi ya kujipima nguvu na Mathare United ya Kenya kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Simba itamenyana na Azam katika mechi ya Ngao ya Jamii ya kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Septemba 8, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Habari za ndani kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zimesema kwamba, kuchelewa kwa mechi hiyo ambako kumeenda sambamba na kuchelewa kuanza kwa ligi hiyo, kumetokana na kuchelewa kufikiwa mwafaka mapema wa mkataba mpya wa udhamini wa Ligi Kuu.

Wakati huo huo, Mshindi wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Azam FC Jumamosi watamenyana na Transit Camp kwenye Uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Kihistoria hiyo itakuwa mechi ya tano ya Ngao ya Jamii kuchezwa nchini na ya pili kuishirikisha timu nje ya wapinzani wa jadi wa soka ya Tanzania, Simba na Yanga.
Mtibwa ilicheza na Yanga mwaka 2009, baada ya Simba kugoma na ikashinda mabao 2-1 na kutwaa Ngao, wakati kabla ya hapo, mwaka 2001, Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa bado inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager, ilichezwa mechi ya kwanza ya Ngao kihistoria.

Katika mechi hiyo, Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Simba na mwaka juzi Yanga iliifunga tena Simba kwa penali 3-1 kufuatia sare ya 0-0 na mwaka jana, Simba ilitwaa Ngao ya kwanza katika historia yake, kwa kuifunga Yanga mabao 2-0.


MABINGWA WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:
Mwaka Mshindi Matokeo
2001 Yanga 2-1 Simba
2010 Yanga 0-0 Simba (3-1penalti)
2011 Simba 2-0 Yanga

Chanzo: http://bongostaz.blogspot.com

IJUMAA YA LEO KATIKA MAGAZETI











PAUL KAGAME ALIVYOWAKARIBISHA YANGA KWENYE IKULU YA RWANDA


Raisi wa Rwanda Paul Kagame akisalimiana na Mama Fatma Karume aliyeomgozana na Yanga kwenda nchini Rwanda.

Kocha wa Yanga Saintfield akisamiliana na Kagame

Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji akisoma risala yake mbele ya Raisi Kagame

Wachezaji wa Yanga wakisikiliza kwa makini risala ya mwenyekiti wao

Nahodha wa Yanga na kocha wakimkabidhi kombel la Kagame - mdhamini mkuu wa kombe hilo Raisi wa Rwanda Paul Kagame.

Mama Karume na Seif Magari wakimkabidhi Kagame jezi ya Yanga

Paul Kagame akiongea na Wachezaji wa Yanga



Mchezaji Mbuyi Twite akiwa na wachezaji wenzie wa Yanga Ikulu ya Rwanda walipoalikwa na Raisi Paul Kagame.

PICHA ZOTE ZIMEPIGWA NA SALEHE ALLY WA CHAMPION

Israili na Afrikan Kusini yazozana


Rais jacob Zuma
Rais jacob Zuma
Israili imekasirishwa na uwamuzi wa serikali ya Afrika ya Kusini wa kupiga marufuku nembo zinazowekwa kwenye bidhaa ambazo zina nembo isemayo ''made in Israel'' il hali zimetengenezwa Ufuko wa magharibi.
Badala yake Afrika ya Kusini inataka bidhaa hizo zibainishwe kwa kuandikwa kuwa zimetengezwa katika ''maeneo yanayokaliwa''
Wizara ya mashauri ya nje ya Israil itaja hatua hiyo kama ya ubaguzi.
Makaazi, miji ya Israili iliyojengwa katika maeneo yanayozozaniwa ya wa Palestina ni kinyume cha sheria ya Kimataifa ingawa Israili inapinga hilo.
Afrika ya Kusini inaaminika kuwa nchi ya kwanza kujaribu kutimiza uamuzi huu kisheria ingawa serikali nyingine kama Uingereza, zimewahi kuyashauri maduka makubwa yabainishe bidhaa zitokazo kwenye makaazi ya walowezi wa Israili.
Lakini kuanzia leo nchini Afrika ya Kusini, bidhaa kutoka makaazi hayo ya Israili, hazitokubalika kuwa na nembo "made in Israel".
Wizara ya mashauri ya nje ya Israili, imeutaja uwamuzi huo kama wa Ubaguzi wa rangi na usiokubalika.
Wizara hiyo imemtaka Balozi wa Afrika ya kusini nchini Israili aeleze hatua ya serikali yake.
Kuna kampeni inayofanywa miongoni mwa wa Palestina na waungaji mkono wao ya kususia bidhaa zinazotengenezwa ndani ya maeneo yanayokaliwa na walowezi wa Kiyahudi pamoja na Israili kwa ujumla.
Msemaji wa vuguvugu la Afrika ya Kusini ameutaja uamuzi wa Afrika ya Kusini kama ishara tu lakini akaonyesha matumaini utakua chachu kwa wengine.
Raia wa Palestina wanaopendelea vikwazo mara kwa mara hutumia mfano wa juhudi za uhuru huko Afrika ya Kusini kama changamoto na kuishutumu Israili kuwa inaendesha sera ya ubaguzi na kuongoza dola la kiimla, Israili inapinga tuhuma hizo.

Taharuki nchini Kenya baada ya mauaji

Baadhi ya watu wamelazimika kutafuta hifadhi sokoni kwa kuhofia usalama wao.

Tana River, Kenya
Tana River, Kenya
Mauaji hayo yalitokea wakati watu wenye silaha kutoka jamii ya Pokomo waliposhambulia kijiji kimoja katika eneo la Reketa huku wakiteketeza makaazi ya watu.
Mmoja wa wale walioathiriwa ameelezea BBC kwamba walishambuliwa usiku, ''hata tumekimbia kutoka kijiji chetu sasa. Walikuja kwa kijiji cha Riketa, watu walikuwa wanalala hata hawana habari wakavamia akina mama, watoto wote wamekufa hapa hapa.''
Alisema shambulizi hilo limewashangaza kwa sababu hata wakati mifugo wao wameingia kwenye mashamba, kuna njia ya kufidia, ''sisi kawaida yetu, hiyo mifugo inashikwa kisha unalipishwa. Sio kukatakata mifugo au kumaliza wachungaji.''
Naibu kamanda wa polisi mjini Mombasa, Joseph Kitur amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa shambulio hilo lilifanywa na watu kutoka jamii ya Pokomo.
Jamii za Pokomo na Orma zimekuwa zikizozania malisho na maji tangu mwezi uliopita lakini shambulizi hili ndilo mbaya zaidi kutokea kati yao.
Mwaka wa 2001, karibu watu 130 walifariki wakati mzozo kati ya jamii hizo mbili ulipozuka.
Jamii ya Pokomo ni wakulima na huwa inategemea sana mto wa Tana kwa shughuli zao.
Jamii ya Orma ni wafugaji.
Mauaji hayo yameleta kumbukumbu za ghasia za baada ya uchaguzi za mwaka wa 2007, ambapo watu 1,200 walifariki katika mapigano.

Uingereza yaibembeleza Ecuador

Uingereza imeandika barua kwa ubalozi wa Ecuador mjini London ikitaka kurejelea mazungumzo kuhusu hatma ya Julian Assange, mwanzilishi wa mtandao wa kufichua siri wa Wikileaks, aliyetorokea katika majengo ya ubalozi huo kuepuka kurejeshwa nchini Sweden kwa lazima.

Julian Assange katika ubalozi wa Ecuador
Uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ulivurugika baada ya uamuzi wa Ecuador kumpa bwana Assange hifadhi ya kisiasa na Uingereza kutishia kuvamia ubalozi huo na kumkamata.
Afisi inayoshughulika na masuala ya kigeni haijasema chochote kuhusu ujumbe uliokop kwenye barua hiyo lakini afisa mmoja ameelezea kuwa inanuia kutuliza hali kati ya mataifa hayo mawili.
Rais Rafael Correa ameiambia BBC kuwa Uingereza ilifanya makosa makubwa kwa kutishia kuingia kwa nguvu kwenye ubalozi wa Equador,''Huu ni mvutano ambao ungeisha iwapo Uingereza ingetoa hakikisho ya kupita kwa usalama kwa Bwana Assange au unaweza kuendelea kwa miezi na hata miaka iwapo hataweza kutoka kwenye ubalozi wetu hapa London kuelekea Equador.''
Huenda mataifa ya Amerika Kusini yakamuunga mkono rais Rafael Correa.
Huku Uingereza ikisema kuwa inataka kurejelea mashauriano kuhusu hatma ya Julian Assange, Equador haikubaliani na msimamo huo na inataka kuhakikishiwa kuwa Assange hatakamatwa iwapo atatolewa kwenye ubalozi wao nchini Uingereza kuelekea Equador.
Equador inataka pia kuhakikishiwa kuwa mwanzilishi huyo wa mtandao wa Wiki Leaks hatawahi kupelekwa Marekani anakokabiliwa na tuhuma za kutoa taarifa muhimu na za siri kwenye mtandao wake.
Hata hivyo hakuna matumaini kwamba Marekani itakubali hilo.
Kwa hiyo ubalozi wa Equador umekiri kuwa huenda ukampa bwana Assange hifadhi kwa miaka mingi.

Chelsea 4-2 Reading: Hazard bags three assists as Blues come from behind to claim victory


Fernando Torres scored the decisive goal as Chelsea came from behind to beat Reading 4-2 at Stamford Bridge.
Frank Lampard opened the scoring with a powerful first-half penalty after Eden Hazard, who impressed once again, had been tripped by Chris Gunter.

Reading equalized shortly after through a thunderous Pavel Pogrebnyak header, before Petr Cech let a Danny Guthrie free kick squirm from his grasp and into his own net.

But Adam Federici followed suit, allowing a Gary Cahill shot to skid away from him, and with less than 10 minutes remaining, Torres was left with the simplest of finishes after good work by Juan Mata and Ashley Cole.

Branislav Ivanovic swept into an open goal in stoppage time, with Federici out of his area after attacking a corner.

Hazard, who had caught the eye in his Premier League debut against Wigan and had three assists against Reading, was involved inside two minutes, racing onto a pass from Mata on the left hand side, but the Belgian’s shot across goal failed to find the target and rolled wide.

Just five minutes later Chelsea went closer, as a lovely fluid passing move involving Torres and Branislav Ivanovic launched an attack for the returning Ramires, but the midfielder chose to test Adam Fedrici rather than play the Chelsea striker in with the goal at his mercy, and the Reading keeper palmed the ball away.

Reading launched a counterattack from Federici’s save, but lone striker Pavel Pogrebnyak flashed his shot wide, before Torres would get his first chance of the match.

The Spain international displayed some excellent trickery to deceive Jem Karacan and Kaspars Gorkss to make space in the penalty area, but his shot was blocked and flew to safety.

It was more Chelsea skill that would create the chance for the opening goal, as Hazard had his standing leg tripped in the box by Gunter, leaving match official Lee Mason with the easy decision to award the penalty.

Lampard stepped up and drilled low and powerfully to Federici’s right and, though the shot stopper dived the right way, he had little chance of keeping the spot kick out.

The home side’s lead lasted little more than five minutes though, as Pogrebnyak headed Reading level.

Garath McCleary exchanged a quick one-two with Danny Guthrie before finding the Russian, who showed expert movement to beat Gary Cahill and head into the top corner beyond Cech.

And, just before the half-hour mark, the visitors were in front after John Terry gave away a free kick for a foul on Jobi McAnuff around 20 yards from goal.

Guthrie blasted low and hard at Cech, but the 30-year old spilled a regulation save and could only watch the ball trickle into his net.

Chelsea had chances to equalize before the interval but Hazard fired over from distance before crossing for Torres, who nodded just wide, while Alex Pearce was inches away from extending the visitors’ lead, but could not connect with an Ian Harte free kick.

The Blues wasted no time in attempting to get back into the game after the break as Torres pulled back to the edge of the box for Ivanovic, but the defender’s shot sailed a long way over the bar.

But, with his side unable to break Reading down in the early stages of the second half, Roberto Di Matteo handed Oscar his Stamford Bridge debut, in place of compatriot Ramires.

Oscar was immediately among the action, nicking the ball away from Karacan, who upended the Brazilian and picked up a yellow card.

With over an hour played, Chelsea was finally able to carve out a second-half opening and after some pinball in the box following an Ivanovic pass, the ball fell to Hazard, but his shot was blocked by Pearce when Federici may well have been beaten.

Di Matteo was forced into another change as the hosts chased the elusive equalizer and replaced John Obi Mikel with Daniel Sturridge.

But it was a defender who would pull the scores level in the 70th minute, when Cahill’s speculative long-range effort bounced in front of the outstretched palms of Federici, who pushed the stinging shot into the bottom corner.

The equalizer appeared to have given Chelsea the impetus to press for a winner, with Juan Mata going close with a shot, beating Federici but curling wide.

And it was Mata again who went close with ten minutes remaining, scuffing wide after an Ivanovic cross cannoned into his path.

Just moments later though, Chelsea scored the winner as Ashley Cole darted onto a pass inside the box and squared for Torres, who got ahead of the resolute Reading backline and tapped into an empty net.

There were suspicions of offside surrounding the goal, but Chelsea took the three points in its first home game of the season as Federici came up for a corner and left his goal exposed, allowing the hosts to break through Hazard, who gifted Ivanovic an open goal

Barcelona 3-2 Real Madrid: Xavi clinches narrow first-leg triumph

Tito Vilanova's first Clasico ended on a mixed note, as a howler from Victor Valdes gifted the visitors a late goal and leaves the second leg of the Supercopa on a knife edge

Cristiano Ronaldo, Dani Alves - FC Barcelona v Real Madrid
Getty Images
Barcelona drew first blood against Real Madrid in the battle for Spanish supremacy this season, narrowly defeating its great rival 3-2 in the first leg of their Supercopa clash at Camp Nou on Thursday.

A cagey first half saw the home side dominate the ball, but struggle to find a way through a resilient rearguard effort from Jose Mourinho's men.

But the match changed completely in the second-half, as Cristiano Ronaldo gave the visitors a shock lead in the 55th minute with a header from a corner.

Barca would hit back instantly through Pedro, before a Lionel Messi penalty and a beautifully worked goal from Xavi put the club in the driving seat.

However, a moment of madness from Victor Valdes gifted Angel Di Maria a goal with five minutes to go, leaving matters finely poised for the second leg in six days at Santiago Bernabeu.
Tito Vilanova dropped Christian Tello to the bench for Alexis Sanchez, despite the former’s impressive performance in the 5-1 win over Real Sociedad last weekend, but new signing Alex Song did not make the match day squad in time.
Mourinho, meanwhile, drafted in Raul Albiol in the center of defense for the injured Pepe, while Karim Benzema started as the lone striker ahead of Gonzalo Higuain.
Madrid started brightly, but was not able to sustain it for long as Barca began to assert its dominance in the middle of the park, with Andres Iniesta in particular looking lively.
Xabi Alonso picked up a yellow card 12 minutes in after a crunching tackle on Sergio Busquets, putting him on thin ice for what was shaping up to be a backs to the wall game for the visitors.
Messi should have found the target in the 19th minute after latching on to Dani Alves’ cutback just inside the box, but his effort flew the wrong side of the post.
The Argentine would miss an even better chance 10 minutes later, poking wide from a good position after dancing around two defenders in the area.
But despite being starved of the ball, Madrid proved a stubborn beast to overcome at the back, as every Barca attack was met by a throng of white shirts in defense.
The match seemed to be settling into a war of attrition, though Pedro almost livened things up on the half-hour mark with a swerving shot that forced Casillas to save at full stretch.
The home fans were up in arms in the 38th minute though, after a theatrical tumble from Sanchez from a challenge by Fabio Coentrao in the box went unacknowledged by the referee.
It was a hopeful shout at best, and the game began to get scrappy as the first half ended. First, Arbeloa was shown yellow for flattening Busquets, before Javier Mascherano joined him in the book after chopping down Coentrao.
Busquets was not having an easy time in the middle of the park, and was felled again by Albiol shortly after the restart, for which the Madrid defender also saw yellow.
The Barcelona midfielder would then make a fatal error in the 55th minute, as he lost sight of Ronaldo defending a corner, allowing the Portuguese to not the visitors into a surprise lead.
Madrid’s joy lasted only seconds though, as straight from kickoff, Barca drew level.
Mascherano’s searching ball from his own half picked out Pedro on the left, who accelerated away from Coentrao to slot the hosts back on terms, despite calls from the visitors for offside.
The shackles were finally off, as Barca looked to press ahead. Alves was picked out by Messi on the overlap, only for Casillas to tip his low shot around the post.
Then, with 68 minutes gone, a clumsy tackle by Sergio Ramos brought down Iniesta in the area, giving referee Carlos Gomez no choice but to point to the spot. Messi stepped up to send Casillas the wrong way and put Barcelona back in front.
Xavi appeared to put matters beyond any doubt 10 minutes later after slotting home from a superb setup from Iniesta, who ghosted pass multiple challenges before putting the chance on a plate for his midfield colleague.
However, in the 85th minute, a howler from Valdes dragged Madrid back into the game and the tie.
The Barcelona keeper appeared to be under little pressure when collecting a backpass, but saw the ball stick under his feet, allowing Di Maria enough time to steal in and poke into the back of the net, giving the visitors a lifeline for the second-leg.

BBC Dira Ya Dunia-Press Release



 Salim Kikeke Ndiye mtangazaji wa kipindi hiki
                                                                       

                    BBC Idhaa ya Kiswahili kuzindua Dira ya Dunia kupitia Star TV nchini Tanzania

23 August 2012. Katika mpango mkubwa wa kutanua wigo wake wa wasikilizaji na watazamaji barani Afrika, BBC imetangaza kuzindua kipindi chake cha kwanza cha habari za dunia kwa lugha ya Kiswahili kiitwacho Dira ya Dunia. Kuanzia Jumatatu Agosti 27, kituo shirika cha BBC Idhaa ya Dunia nchini Tanzania, Star TV, kitarusha kipindi cha Dira ya Dunia cha BBC Idhaa ya Kiswahili. Matangazo hayo ni ya dakika 30 yakiwapa watazamaji fursa ya kupata habari motomoto za dunia na uchambuzi yakinifu kutoka katika shirika hilo la utangazaji la kimataifa ulimwenguni.

Kipindi hicho ambacho kitakuwa kikirushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa kitatoa chachu katika matangazo ya Star TV kwa kuwaletea watazamaji habari za kiwango cha hali ya juu kutoka katika kitovu cha habari za dunia cha BBC- Global News. Dira ya Dunia pia itawaletea watazamaji taswira na uchambuzi yakinifu kutoka kwa waandishi wa habari waliotapakaa katika nchi 48 barani Afrika, na hivyo kuleta picha halisi ya bara zima kwa watazamaji wanaozungumza Kiswahili.

Kipindi cha radio cha Dira ya Dunia ni kipindi maarufu sana kwa mamilioni ya wasikilizaji katika eneo la Afrika Mashariki na Kati na hata wasikilizaji wanaoishi nje ya eneo hilo. Kwa kuzindua kipindi cha TV chenye jina kama hilo, BBC ina imarisha zaidi matangazo yake hasa kwa kutumia waandishi wake wa habari waliobobea – watangazaji Salim Kikeke na Charles Hilary, mhariri Mariam Omar pamoja na waandishi waliopo Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Kenya, Nigeria, Rwanda, Afrika Kusini, Sudan Kusini, Tanzania, Uganda na Uingereza.

Mhariri wa BBC Idhaa ya Kiswahili, Ali Saleh anasema: “Uzinduzi wa Dira ya Dunia kupitia TV, ni kwenda na mabadiliko makubwa tunayoyashuhudia ya jinsi watu wanavyofuatilia habari barani Afrika, na pia mahitaji wa mashabiki wa BBC Ihdaa ya Kiswahili. Tunavyoarifu na kuchambua habari za eneo letu na hata duniani, iwe siasa, uchumi au utamaduni, Dira ya Dunia itatoa taswira halisi ya Afrika, tofauti na jinsi ambavyo bara hili limekuwa likiripotiwa kwa miaka mingi. Kipindi chetu kitakuwa kinashirikisha watazamaji, na pia kuzigatia misingi ya BBC ya muda mrefu ya uhuru, uhakika na bila upendeleo”

Kinara wa Dira ya Dunia, Salim Kikeke ameongeza kwa kusema: “Ni heshima kubwa na nafasi ya kipekee kuwa katika mradi huu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC wa TV. Tumepitia mengi hadi kufika hapa, na kila sekunde ya safari hiyo ilikuwa ni ya kuvutia.Ni imani yangu kuwa kipindi hiki kipya cha TV kitavutia wengi katika eneo la Afrika Mashariki na Kati.”

Uanzishaji wa Dira ya Dunia katika TV ni sehemu ya mabadiliko makubwa ya matangazo yaliyofanyika ndani ya BBC mwaka huu katika bara la Afrika, katika TV na redio. Uzinduzi huu umekuja muda mfupi baada ya kuzinduliwa kwa kipindi cha TV kwa lugha ya Kiingereza kwa Afrika, Focus on Africa, ambacho pia kinarushwa kupitia Star TV. Mwezi Julai, siku chache kabla ya kuanza kwa michuano ya Olimpiki jijini London, BBC Idhaa ya Ulimwengu ilizindua kipindi kipya cha redio, Newsday – Kipindi ambacho kimelenga zaidi wasikilizaji wa redio wa asubuhi barani Afrika.

Mhariri wa BBC wa eneo la Afrika, Solomon Mugera, naye amesema: “Miongo mingi ya utangazaji katika lugha mbalimbali barani Afrika, BBC imejenga uhusiano wa kipekee na wasikilizaji wetu wa redio, kwa kueleza ya Afrika duniani, na kuipeleka dunia barani Afrika. Kukua kwa njia za utangazaji za BBC ni ushahidi wa kuwepo kwa mizizi ya muda mrefu na ufahamu wa bara la Afrika. Tunavyoanza safari hii mpya, kwa kweli tuna hamasa kubwa hasa kwa kushirikiana na mashirika ya utangazaji yenye hadi kubwa katika eneo letu.”

Nathan Lwehabura, Meneja mipango na utafiti wa SMG Ltd, anasema: “ Ni heshima kubwa kwa Star TV kujumuisha Dira ya Dunia katika vipindi vyake vya kila siku – tunaamini kipindi hiki kitavutia watu wengi. Kipindi cha BBC cha Kiingereza kilichozinduliwa hivi karibuni kupitia Star TV, Focus on Africa, kinazidi kujipatia umaarufu mkubwa, sio tu miongoni mwa watazamaji wetu, bali pia hata miongoni mwa mashirika mengine kutokana na kuzingatia fani ya uandishi, utangazaji na ubora wa kipindi. Ni matumaini yetu kuwa ushirika kati ya BBC na Sahara Media Group utaimarisha matangazo yetu ya TV hasa tunavyoelekea katika matangazo ya kisasa ya mfumo wa digital.”

Dira ya Dunia kutoka Idhaa ya Kiswahili ya BBC itakuwa ikitangazwa Jumatatu hadi Ijumaa, saa tatu usiku kupitia Star TV nchini Tanzania. Pia matangazo hayo yatapatikana kupitia wavuti wa BBC Idhaa ya Kiswahili – bbcswahili.com.

BBC ilirusha matangazo yake ya kwanza kabisa barani Afrika zaidi ya miaka 80 iliyopita. Idadi kubwa ya wasikilizaji kwa ujumla kupitia redio na TV inaifanya BBC kuwa shirika kubwa zaidi la kimataifa la utangazaji barani Afrika.

Kwa taarifa zaidi tafadhali wasiliana na:

BBC Global News Press Office
+44 207 557 2944; sophie.west@bbc.co.uk


Kwa wahariri:

BBC Idhaa ya Kiswahili ni watangazaji wa habari kupitia TV, redio na kwenye mtandao kwa lugha ya Kiswahili na kwa wasikilizaji na watazamaji wa lugha hiyo. Matangazo ya redio kwa Kiswahili yanapatikana kupitia vituo vya redio vya FM na pia kupitia redio washirika nchini Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Kenya, Malawi, Mozambique, Rwanda na Uganda. Matangazo pia yanapatikana kupitia wavuti bbcswahili.com ambapo pia habari mpya kabisa zinapatikana, makala na uchambuzi kuhusu Afrika Mashariki na pia duniani kote, kwa maandishi, sauti na video.

BBC Idhaa ya Kiswahili ni sehemu ya BBC Idhaa ya Dunia (BBC World Service), ambao ni watangazaji wa kimataifa wanaotoa huduma ya matangazo kwa lugha mbalimbali kupitia redio, TV na kwenye wavuti na pia kupitia vifaa vitumiavyo visiwaya. Kwa taarifa zaidi tembelea bbcworldservice.com

BBC ina mashabiki milioni 239 kwa wiki duniani kote katika huduma zake za habari za kimataifa ikiwemo BBC World Service, BBC World News TV na bbc.com/news.

Taswira Zaidi Uzinduzi Wa BBC-Dira Ya Dunia Na Star TV

 Salim Kikeke mtangazaji wa kipindi
 Meneja wa Sahara Media Group
 Watangazaji wa BBC na wa Star TV
 Viburudisho
Jana kwenye hotel ya Harbour View