Tuesday, August 7, 2012

Keita aondoka Barcelona

Mchezaji wa kiungo wa Mali Seydou Keita amekihama klabu cha Barcelona baada ya kukichezea kwa miaka minne.
Seydou Keita na wenzake wakisheherekea ushindi
Katika muda huo wa miaka minne, Keita aliisaidia Barcelona kuzoa jumla ya vikombe 14.
Wakati wakithibitisha kuondoka kwa mwamba huyo, Barca walimishukuru Seydou Keita kwa juhudi zake za kuletea klabu hicho cha Uhispania mafanikio na vile vile wakamtakia kila lakheri anakokwenda.
Kwa wakati huu kuna fununu kwamba mchezaji huyo wa Mali huenda anahamia klabu kimoja cha Uchina, Dalian Aerbin
Ikiwa hatiamae ataishia China basi Keita hatakuwa mchezaji wa kwanza kutoka bara la Afrika kufanya hivyo.
Majuzi nahodha wa timu ya Ivory Coast Didier Drogba aliwafuata Frederic Kanoute na Yakubu Aiyegbeni wa Nigeria kujiunga na timu za ligi kuu ya China.
Keita, mwenye umri wa 32, alijiunga na Barcelona mwaka 2008 kutoka Sevilla akiwa ni mchezaji wakwanza kabisa ambaye Pep Guardiola alimsajili mara tu alipochukuwa uongozi wa Barca.
Kabla ya hapo mchezaji huyo alikuwa Olympic Marseille, Lorient na Lens zote za Ufaransa na ndio baadaye akahima Seville ya Uhispania.
Keita amehama baada ya Guardiola luondoka kama Meneja wa Barcelona na mahali pake kuchukuliwa na aliyekuwa naibu wake Tito Vilanova

USAIN BOLT NOUMA

Usain Bolt ameanza vyema juhudi zake za kuchukua tena medali nyingine ya dhahabu katika mbio fupi za mita 200, huku akiwa tayari akiwa na ile ya dhahabu katika mbio za mita 100.
Usain Bolt
Anatazamiwa kuweka kibindoni medali ya mita 200
Bolt alifuzu kuingia mbio za nusu fainali, mita 200, kwa muda wa sekunde 20.39.
Wanariadha wenzake kutoka nyumbani Jamaica, Yohan Blake na Warren Weir pia walifuzu.
Wengine waliofanikiwa kuingia nusu fainali ni Mmarekani Wallace Spearmon, Mfaransa Christophe Lemaitre na Muingereza Christian Malcolm.
Muingereza James Ellington alishindwa kufuzu kuingia nusu fainali, baada ya kumaliza katika nafasi ya sita.
Mbio za nusu fainali mita 200 ni Jumatano, na fainali ni Alhamisi.
Bolt, bingwa mara nne katika mashindano ya Olimpiki, na aliyefanikiwa kuutetea ubingwa wake wa mjini Beijing kikamilifu Jumapili katika mbio za mita 100, atajaribu tena kuhifadhi ubingwa katika mbio za mita 200 pia.
Akizungumza na waandishi wa michezo wa BBC, Bolt alisema: "Kuna mashabiki wa ajabu, na wana jukumu muhimu sana katika mbio ninazoshiriki, na mimi huzipenda sana mbio za mita 200".
"Mimi hujaribu kutimiza wajibu wangu, ninaelewa kila kinachofuatia ushindi, kwa hiyo ni lazima nifurahie kile ninachokifanya".
Blake, ambaye alipata medali ya fedha kwa kumaliza wa pili nyuma ya Bolt katika mbio za mita 100, pia alifuzu vyema kuingia nusu fainali ya mbio za mita 200, akiandikisha muda wa sekunde 20.38.
Blake alielezea: "Ninajihisi nimo katika hali nzuri mno. Yote ni kutokana na kocha, na mbio za mita 100 zimenifundisha mengi."
"Ilikuwa ni medali yangu ya kwanza katika mbio za Olimpiki. Mimi hufurahia zaidi mbio za mita 200, na ninaweza kuvumilia zaidi muda huo mrefu."

PICHA YA SIKU: MAPACHA WAWILI - SOKA SIO VITA NI USHINDANI


Wabunge wa Kenya waketia viti vipya

Viti vipya vya bunge
Bunge la Kenya lililokarabatiwa na ambalo limekuwa gumzo kubwa kwa sababu ya gharama ya viti vya bunge hilo, hatimaye limefunguliwa rasmi na rais wa nchi hiyo Mwai Kibaki.
Viti hivyo vimegharimu dola 3,000 za kimarekani kwa kila kiti kimoja vikiwa jumla ya 350 vimetengenezwa na kitengo cha magereza nchini humo.
Zabuni ya kwanza ya kutengeneza viti hivyo ilitolewa kwa kampuni moja ya nje lakini ilifutwa baada ya baadhi ya wabunge kugundua kila kiti kingegharimu dola 5000 za kimarekani.
Maafisa wanasema ukarabati huo uliogharimu dola milioni 12 utaliweka bunge katika mfumo mpya wa kisasa wa komputa.
"Mabadiliko tunayoyafanya yataleta mabadiliko chanya katika uongozi," spika wa bunge Kenneth Marende ameiambia BBC.
Amesema mfumo wa kupiga kura wa elektroniki utawawezesha wabunge kupiga kura kwa uhuru wao binafsi kuliko kulazimika kupiga kura kwa kuhofia vyama vyao.
"sasa mbunge atakuwa peke yake, huru kabisa binafsi, atafanya maamuzi yake na kubonyeza tu kitufe."
Mwandishi wa BBC Odeo Sirari mjini Nairobi, anasema baadhi wanaona viti hivyo kuwa ni vya gharama kubwa sana kuliko mabunge mengine katika jumuiya ya madola.
Waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga na rais Mwai Kibaki pamoja na wabunge ni miongoni mwa wanaolipwa mshahara wa juu sana barani Africa.
Wabunge walifurika katika jengo hilo lililokarabatiwa wakati rais na spika wakiongoza utaratibu wa sherehe za ufunguzi.
Ukarabati huo ulianza mwezi Aprili mwaka 2010 na ulikuwa umepangwa kuchukua mwaka mmoja kumalizika lakini ulichelewa kwasababu ya utata ulioghubika zabuni yake, mwandishi wetu anasema.
Bunge la zamani
Mbunge John Mbadi, katika kamati ya uwekezaji aliongoza upinzani juu ya zabuni ya kwanza.
"hatukuweza kuelewa ni kwa vipi wabunge wangekuwa wanakaa katika viti vinavyogharimu karibu shilingi 400,000 za Kenya kama dola 5,000, ambazo kwa kiwango chochote cha kawaida zingeweza kujenga nyumba kwa wananchi kadhaa," ameiambia BBC.
"ilikuwa ni upuuzi," amesema.
Mwandishi wetu anasema watu wengi wamelalamika kuwa gharama za sasa bado ni juu.
David Langat, anayesimamia uzalishaji katika magereza nchini Kenya, amesema vifaa vyote vilivyotumika vilitoka nchini Kenya lakini gharama za viti zimekuwa kubwa sana.
Ameiambia BBC kuwa viti hivyo vyenye uzito wa kilo 50 kila kimoja vina kinga dhidi ya moto na vina dhamana ya miaka 30.
Kwa sasa Kenya ina jumla ya wabunge 220 lakini ukumbi huo umewekwa viti 350 idadi ambayo watachaguliwa katika uchaguzi ujao mwezi Machi kwa mujibu wa katiba mpya.

JK Kwenye Ziara Ya Kikazi Uganda


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rubani Bomani na wanaanga wenzie  wa Ndege za Serikali  kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuu asubuhi leo Agosti 7, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mnadimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi la Tanzania  Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo  kabla ya kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuuasubuhi leo Agosti 7, 2012. Katikati yao ni Inspoekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Mhe Saidi Mecky Sadik  kabla ya kuanza safari ya kwenda Kampala, Uganda,kuhudhuria mkutano wa nchi za Maziwa Makuu asubuhi leo Agosti 7, 2012
PICHA NA IKULU

MADAKTARI KUJADILI HALI YA DR. ULIMBOKA

                                                               
Fidelis Butahe 
WAKATI kukiwa na taarifa za kurejea nchini kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka viongozi wa Jumuiya hiyo na Umoja wa Madaktari Tanzania (MAT), wanatarajia kukutana leo kujadili mkanda mzima wa sakata lililomkumba kiongozi huyo.  Baada ya kikao hicho, madaktari hao watakutana na familia yake na kisha kumuuliza Dk Ulimboka kama angependa kilichomtokea kiwekwe wazi kwa jamii.

 Dk Ulimboka ambaye alikuwa anaratibu mgomo wa madaktari uliokuwa ukiendelea nchi nzima, alitekwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Jumatato ya Juni 27 mwaka huu na kupelekwa katika msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji a Dar es Salaam, ambako aliteswa na kujeruhiwa vibaya.

Katika tukio hilo daktari huyo aling’olewa meno mawili na kucha za mkono mmoja na baadaye kulazwa katika Kitengo cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalum (ICU) katika Taasisi ya Mifupa (MOI).  Baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya Juni 30 mwaka huu, alisafirishwa kwenda Afrika a Kusini kwa ajili ya vipimo na matibabu.

 Kusafirishwa kwake kulifuatia taarifa ya jopo la madaktari lililokuwa linamhudumia kutoa taarifa kwa madaktari bingwa kuhusu abadiliko ya afya.

 Taarifa za kurejea kwa Dk Ulimboka zimezagaa katika mitaa mbalimbali jijini Dar es Salaam, huku baadhi ya watu wakizijadili katika mitandao ya kijamii.  Akizungumza na gazeti hili Katibu wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Edwin Chitage, alisema kuwa hali ya Dk Ulimboka inazidi kuimarika lakini alisita kueleza wazi ni lini kiongozi huyo wa madaktari atarudi nchini.

 “Tukiwa tayari tutatoa taarifa katika vyombo vya habari juu ya suala zima la afya ya Dk Ulimboka,” alisema Dk Chitage.  Alisema leo au kesho viongozi mbalimbali wa MAT na Jumuiya ya Madaktari, watakutana kujadili suala la kiongozi huyo.

 “Ndani ya siku mbili hizi (leo na kesho) viongozi tutakutana na kujadili ripoti ya matibabu ya Dk Ulimboka na tutajadili kama tuvieleze vyombo vya habari ama laa,” alisema Dk Chitange.  Hata hivyo Dk Chitange alisema hatua hiyo itategemea na kauli ya familia ya Dk Ulimboka na  yeye mwenyewe (Dk ULimboka) kwa kuwa na wao pia watashirikishwa.

 “Dk Ulimboka na familia yake tutawashirikisha katika mambo ambayo tutayajadili,” alisema Dk Chitage.  

    Alipoulizwa kama kiongozi huyo wa madaktari sasa anaweza kufanya shughuli zake kama awali, alisema hana uhakika kwa kuwa hana taarifa za ndani zaidi . CHANZO: MWANANCHI

Cristiano Ronaldo: Topping Goal.com 50 is 'a matter of pride'


                                     

Goal.com's top player for the 2011-12 season accepted his award in Los Angeles, where Real Madrid is currently stationed on a preseason tour.

“It’s a matter of pride for me to win this award," said the two-time Goal.com 50 winner. "I would not have been able to do it without the support of my teammates.”

In a year that saw the former Manchester United player win his first La Liga crown as a member of Los Merengues, Ronaldo capped off a spectacular individual season at the club level by scoring 60 goals across all competitions in 55 games, including 46 strikes in the domestic championship. Ronaldo scored 10 times in the same amount of matches during Real Madrid's Champions League run to the semifinals.

Adding to his monstrous scoring total, Ronaldo also assisted his teammates on 15 occasions, making him one of the team's top passers as well as the main offensive threat.

Since manager Jose Mourinho's arrival in 2011, Cristiano Ronaldo and Los Blancos have won the Copa del Rey and La Liga, with an eventual 11th Champions League title still looming, a trophy Real Madrid has not been able to win since the 2001-02 season.

2011-12 GOAL.COM 50 WINNER:
CRISTIANO RONALDO
The Portuguese superstar has topped our definitive countdown of the finest players from 2011-12. Click here to view our slideshow from 50-1!
“My immediate goals are to work to the fullest with my team in order to fight for all the available championships. I don’t prioritize one because I want to conquer however many I can, but to do that we’ll have to fight our hardest and do it with humility," the striker added.

Following his sparkling club year, Ronaldo led Portugal to a semifinal finish at the Euro 2012 tournament held in Poland and Ukraine, sharing top scoring honors with five other players.

With Ronaldo leading the charge for Euro 2012, Portugal survived the competition's group of death by placing second in Group B with six points, below Germany and above Denmark and the Netherlands.

Ronaldo's second-half goal against the Czech Republic saw the Lusos through and into the semifinal clash against Spain, where they lost to the eventual champion in a penalty shootout.

Looking forward to the 2012-13 season, Real Madrid will wrap up its preseason tour of the United States and end August by clashing with old foe Barcelona for the Spanish Supercopa in what will be the first Clasico of the season.

Real Madrid will also be heavily favored to defend its La Liga title as well as fighting for the Copa del Rey and, of course, the Champions League.

"I’m sure that with such a great group like this, the obstacles in front of us will not seem so daunting,” Ronaldo said.

Official: Arsenal sign Santi Cazorla from Malaga

                            

The Gunners have completed their third signing of the summer, securing the Spain attacking midfielder for a fee of around £18 million

MEMBE: TANZANIA IPO TAYARI KWA TISHIO LOLOTE LA MALAWI

                                                   
SERIKALI imesema eneo linalogombewa na Malawi katika Ziwa Nyasa ni mali ya Tanzania na sasa imeziamuru kampuni za nchi hiyo zinazofanya utafiti wa mafuta kuondoka eneo hilo kuanzia jana.

Onyo hilo dhidi ya Malawi lilitolewa jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye pia amesisitiza kuwa Tanzania itakuwa tayari dhidi ya tishio lolote la dhahiri au la kificho la kiusalama.

Hii ni mara ya pili Serikali kuionya Malawi katika mgogoro huo. Wiki iliyopita aliyekuwa Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni Samuel Sitta alisema: “Tuko tayari kwa lolote dhidi ya Malawi.”

Sitta alitoa kauli hiyo alipokuwa akijibu Swali la Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu mgogoro huo.

Jana, akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2012/13, bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisisitiza kwamba eneo linalobishaniwa katika ziwa hilo lipo Tanzania.

Alisema pamoja na Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuzipiga marufuku ndege za utafiti za kampuni hizo, bado zilikaidi na ndege tano zilitua katika eneo la Ziwa Nyasa.

“Serikali ya Tanzania inapenda kuzionya na kuzitaka kampuni zote zinazoendelea na shughuli za utafiti katika eneo hilo zisitishe mara moja kuanzia leo (jana),” alisema Membe.Alisema Serikali ya Tanzania iko tayari kulinda mipaka yake kwa gharama yoyote na haitaruhusu utafiti huo wa uchimbaji wa gesi na mafuta uendelee.

Alisema chini ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wananchi wa Tanzania watakuwa salama dhidi ya tishio lolote la dhahiri au la kificho la kiusalama.

Kiini cha Mgogoro
Kuhusu kiini cha mgogoro, Waziri Membe huku akirejea historia ya mipaka tangu ukoloni, alisema ni hatua ya Serikali ya Malawi kushikilia msimamo kuwa eneo lote la Ziwa Nyasa lipo Malawi wakati Tanzania inashikilia kuwa mpaka upo katikati ya Ziwa.

“Wenzetu wanadai ziwa lote lipo Malawi lakini, nyaraka zilizotengenezwa na wakoloni wa Kiingereza mwaka 1928 na 1938 zinaonyesha kuwa mpaka wa ziwa hilo upo katikati,” alisema. Alisema hoja ya Tanzania ina nguvu kulingana na sheria za kimataifa kwa vile tatizo kama hilo linafanana na mgogoro uliokuwepo baina ya Cameroon na Nigeria.

Venus,Serena wavunja rekodi ya Olympiki

                                                                     
Wanadada wawili mashuhuri katika mchezo wa tennis Venus na Serena Williams wametetea mataji yao mawili waliyoshinda katika michezo ya Olympiki ya Beijing miaka miine iliyopita kwa ushindi wa seti 6-4 6-4 dhidi ya Andrea Hlavackova na Lucie Hradecka wa Jamhuri ya Chek katika mshindano ya Olympic yanayoendelea jijini London Uingereza.
Ushindi huu unamaanisha kuwa Wamarekani hawa wanakuwa ndio wachezaji wa kwanza katika mchezo wa tennis katika historia ya michezo ya Olympic kuwahi kushinda medali katika mashindano matatu tofauti.
Walifanikiwa kushinda medali katika michezo hiyo ilipofanyika katika miji ya Sydney Australia, Beijing Uchina, na sasa London nchini Uingereza.

NAIBU JAJI MKUU WA KENYA APATIKANA NA HATIA

                                 NANCY BARAZA                         
Jopo maalum la majaji lililoteuliwa na rais Mwai Kibaki kuchunguza tuhuma zilizokuwa zinamkabili Naibu Jaji Mkuu wa Kenya Nancy Baraza kumdhalilisha mlinzi mmoja katika duka moja kubwa mjini Nairobi, imependekeza, jaji huyo kuondolewa madarakani.
Akisoma hukumu hiyo mjini Nairobi leo, mwenyekiti wa jopo hilo, Jaji mkuu mstaafu wa Tanzania, Augustino Ramadhan, amesema Nancy Baraza akiwa mtumishi wa chombo cha kusimamia sheria na haki hakutakiwa kwa namna yoyote kutenda kosa hilo dhidi ya mlalamikaji Bi Rebecca Kerubo.
Amesema kitendo alichofanya Nancy Baraza na ni cha utomvu mkubwa wa nidhamu na hivyo kupendekeza kwa Rais Mwai Kibaki kumwondoa katika wadhifa wake wa naibu jaji mkuu.
Nancy Baraza alituhumiwa kumnyanyasa na kumpiga Bi Kerubo tarehe 31 Desemba 2011, baada ya kutakiwa kufanyiwa ukaguzi kabla ya kuingia katika duka hilo, utaratibu ambao umekuwa ukitekelezwa kwa wateja wote.

OXFAM YAHUZUNIKA HALI YA KIVITA CONGO


Viongozi wa mataifa ya maziwa makuu kukutana mjini Kampala kujadili mzozo uliopo mashariki mwa DRC. dakika 58 zilizopita