Tuesday, August 7, 2012

Venus,Serena wavunja rekodi ya Olympiki

                                                                     
Wanadada wawili mashuhuri katika mchezo wa tennis Venus na Serena Williams wametetea mataji yao mawili waliyoshinda katika michezo ya Olympiki ya Beijing miaka miine iliyopita kwa ushindi wa seti 6-4 6-4 dhidi ya Andrea Hlavackova na Lucie Hradecka wa Jamhuri ya Chek katika mshindano ya Olympic yanayoendelea jijini London Uingereza.
Ushindi huu unamaanisha kuwa Wamarekani hawa wanakuwa ndio wachezaji wa kwanza katika mchezo wa tennis katika historia ya michezo ya Olympic kuwahi kushinda medali katika mashindano matatu tofauti.
Walifanikiwa kushinda medali katika michezo hiyo ilipofanyika katika miji ya Sydney Australia, Beijing Uchina, na sasa London nchini Uingereza.

0 comments:

Post a Comment