Thursday, August 16, 2012

Mzozo wa ziwa Nyasi kujadiliwa leo


Rais wa Tanzania

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Rais wa Malawi Joyce Banda hii leo anaelekea jijini Maputo, nchini Msumbiji, kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC, ambako anatazamiwa kukutana na Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, ili kuzungumzia utata unaozunguka umiliki wa ziwa Nyasa katika mpaka wa mataifa ya Malawi na Tanzania.
Wakati hayo yakisubiriwa serikali ya Tanzania, imeendelea kusisitiza kuwa ni lazima mzozo uliopo kati yake na Malawi kuhusu umiliki wa ziwa hilo umalizwe kwa mazungumzo na sio kutumia nguvu.
Lakini kwa upande wake serikali ya Malawi imepuuuza wito huo wa serikali ya Tanzania na kusisitiza kuwa, ziwa hilo lote ni la Malawi hivyo utafiti wa mafuta utaendelea.

0 comments:

Post a Comment