Thursday, August 16, 2012

SIMBA B YALIPA KISASI KWA AZAM FC NA KUTINGA FAINALI SUPER8 CUP




Timu ya soka ya Simba B imeifunga timu ya Azam katika mchezo wa nusu fainali wa kombe la Super 8 katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Magoli ya Simba yalifungwa na wachezaji Rashid Ismial na Haroun Athumani wakati goli la kufutia machozi la Azam lilifungwa na beki wake wa kutumainiwa Saidi Morad.

Kwa ushindi huo Simba itacheza fainali ya Super 8 siku ya Jumamosi dhidi ya wakata miwa wa manungu Mtibwa Sugar ambao mapema leo waliwafunga Jamhuri ya Pemba mabao 5-1.

Simba leo waliwakilishwa na kikosi cha Abuu Hashimu(18), Miraj Adam (19), Omary Salum (11)/William Lucian ‘Gallas’, Hassan Isihaka (5), Hassan Hatibu (15) Said Ndemla (13), Haroun Athumani (7), Abdallah Seseme (17), Rashid Ismail (8), Edward Christopher (9)/Ramadhan Mzee na Frank Sekule (4)Ibrahim Ajibu.
Benchi; Saleh Malande (1), Ramadhan Mzee (2), William Lucian ‘Gallas’(3), Kenny Alex (12), Mohamed Salum (16), Ibrahim Ajibu (20) na Jesse Nyambo (14).
Makocha: Suleiman Matola. Msaidizi; Amri Said.

Azam FC - Wandwi Jackson (18), Ibrahim Shikanda (21), Samir Hajji Nuhu (11), Said Mourad (15), Luckson Kakolaki (5), Abdulhalim Humud (24), Sunday Frank (12), Jabir Aziz (25)/Khamis Mcha, Gaudence Mwaikimba (17)/Zahor Pazi, Abdi Kassim (20) na Kipre Herman Tcheche (27)Hamisi Mcha.

Benchi; Aishi Mfula (1), Omary Mtaki (2), Himid Mao (23), Khamis Mcha (22), Kelvin Friday (28). Abdulghani Gullam (14) na Zahor Pazi (9).
Makocha: Boris Bunjak (Serbia). Msaidizi; Vivek Nagul (India).

0 comments:

Post a Comment