Thursday, August 16, 2012

Syria yaondolewa kama mwanachama wa OIC


Ekmeledin Ihsanoglu wa OIC

Ekmeledin Ihsanoglu wa OIC
Jumuiya ya muungano wa nchi za Kiislamu (OIC) imesimamisha uanachama wa Syria katika muungano huo.
Baada ya kumalizika kwa mkutano wa viongozi wa Kiislamu uliofanyika mjini Mecca, katibu mkuu wa Muungano huo, Ekmeleddin Ihsa-noglu, alisema muungano huo wa mataifa ya kiislamu hauna nafasi kwa taifa ambalo serikali yake inawaua raia wake.
Hatua hiyo imesababisha kutengwa zaidi kwa Rais Bashar al-Assad baada ya jumuiya ya mataifa ya ki-arabu kuitimua mnamo mwezi Novemba.

0 comments:

Post a Comment